DLIIC katika mchakato wa kutafuta wabunifu ili kupambana na changamoto za afya nchini Tanzania

DLIIC katika mchakato wa kutafuta wabunifu ili kupambana na changamoto za afya nchini  Tanzania

DLIIC katika mchakato wa kutafuta wabunifu ili kupambana na changamoto za afya nchini  Tanzania

Katika kipindi cha miaka kumi iliyopita, Serikali ya Tanzania imekuwa na  maendeleo mazuri katika kufungua vituo vya takwimu ili kuweza kuweka uwazi mkubwa na kuongeza ufanisi kiutendaji. Hata hivyo pamoja na jitihada hizo za serikali  kuna fursa nyingine ya  kuhusisha zaidi jamii na kuijengea uwezo kiufundi kwa kutumia habari ili iweze  kushughulikia kikamilifu vipaumbele vya taifa.

Hadi sasa wabunifu 12 wameweza kupewa ruzuku kwa ajili ya kutafuta ufumbuzi katika masuala  ya afya nchini  Tanzania kupitia mpango wa maalumu unaoitwa  Local Impact Innovation Challenge (DLIIC)  unaofadhiliwa na Serikali ya Marekani kupitia mpango wa dharura wa Rais kwa ajili ya kushughulikia masuala ya UKIMWI  (PEPFAR).

Kupitia mpango huo, Wajasiriamali hawa watapata fedha kuanzia dola za Marekani  7,000 hadi dola 25,000, na msaada wa kiufundi pamoja na  ushauri ili waweze kutekeleza fumbuzi wa aina mbalimbali  katika masuala ya kijamii.

Mapendekezo ya kushindanisha  yanajumuisha ufumbuzi unaofaa kusaidia wananchi kupata habari za huduma za afya, kupunguza upungufu   wanawake na wasichana wadogo mashuleni ambao  unaosababishwa na changamoto za afya, kuwezesha kugawana taarifa juu ya ubora wa huduma za afya, na kuongeza matumizi ya wananchi  ya kumbukumbu za Serikali ya Tanzania (Daftari la Usajili wa Afya au HFR).

Mapendekezo ya kushindanisha yakiwa yameambatanishwa  na jina la kiongozi wa timu kulingana na mada yao kuu  ni kama ifuatavyo:

 

*Upatikanaji wa Huduma za Afya Bora na Taarifa

Jackson Machael Ilangali

Musa Sendama Kamata

Bukhary Haruna Kibonajoro

Rahim Abas Kiobya

George Elly Matto

Mohammad Abdulghany Himidi Msoma

*Maoni kutoka kwa jamii

Steven Edward Mangowi

Rachel Samuel Nungu

*Uwezeshaji kwa wananchi

Lulu Said Ameir

Rose Peter Funja

Jonathan Manyama Kifunda

Josephat Geofrey Mandara

Mapendekezo 12  yalichaguliwa kutoka katika  maombi 129 baada ya kupitiwa na jopo huru la wajasiriamali wa Tanzania, wavumbuzi na wataalamu wa afya kulingana na uwezo wao wa kuboresha aidha au mahitaji ya  takwimu.

Mapendekezo yalitakiwa kuzalisha au kutumia taarifa au takwimu zilizowazi  ambazo zimefanya kazi  ndani ya miezi mitatu, na kuzingatia masuala yanayowakabili vijana, wanawake wadogo na jamii kwa ujumla.

Ufumbuzi wake pia ulitakiwa kulenga angalau moja ya wilaya 84 ambazo zinazingatia vipaumbele chini ya PEPFAR 2017 Mpango wa Uendeshaji wa Nchi Tanzania (COP), ulioandaliwa kwa kushirikiana na Serikali ya Tanzania.

“Mpango huu wa (DLIIC)   una  lengo la kushiriki, kusaidia, na kuunganisha wabunifu wa Watanzania, watengenezaji na watoa ufumbzi kwa kila mmoja na pia kutoa fursa ya kuondoa tofauti katika jamii,” anasema Agapiti Manday ambaye ni  Meneja wa Programu   ya  DLIIC.

DLIIC inakusudia kuwajenga vijana kikamilifu, ili kuimarisha matumizi yao ya takwimu  na uwezo wa sayansi ya takwimu  na kuchangia lengo la PEPFAR  la kuleta ushiriki mkubwa wa wananchi katika kudhibiti, na hatimaye kulimaliza  janga la UKIMWI.

Washindi wataanza mafunzo yao  wiki ya kwanza ya Machi 2017, na watafanya kazi katika kutekeleza miradi yao zaidi ya miezi 3-6.

Watakuwa sehemu ya mpango wa ujasiriamali ambao utaimarisha ujuzi wao wa usimamizi wa miradi, biashara binafsi na uwezo wa kutumia sayansi ya kumbukumbu. Jambo muhimu zaidi kwa  wabunifu hawa watakaoshinda wataweza kusambaza maana ya ubunifu katiika jamii zao  ili kuondoa mambo ambayo yanaathiri  maisha ya Watanzania.

Leave a Reply

Your email address will not be published.